- Sunna ya swala ya rakaa mbili kwa ajili ya salamu ya msikiti kabla ya kukaa.
- Amri hii ni kwa atakayetaka kukaa, atakayeingia msikitini na akatoka kabla ya kukaa, amri hii haimuhusu.
- Atakapoingia mwenye kuswali na watu wakiwa ndani ya swala, akaingia nao, basi hilo litamtosheleza na rakaa mbili.