- Himizo la kuoga siku ya Ijumaa kabla ya kwenda kuswali.
- Fadhila za kuwahi swala ya Ijumaa kuanzia saa za mwanzo wa mchana.
- Himizo la kwenda mbio katika matendo mema.
- Malaika huhudhuria swala ya Ijumaa na kusikiliza hotuba.
- Malaika wako katika milango ya misikiti, wakiwaandikia wale wanaokuja, mmoja baada ya mwingine, wanapokuja kwa ajili ya Swala ya Ijumaa.
- Amesema bin Rajab: Kauli yake: “Mwenye kuoga siku ya Ijumaa kisha akaondoka” Inaashiria kuwa josho lililopendekezwa kwa siku ya Ijumaa linaanza kwa kuchomoza alfajiri, na mwisho wake ni muda wa kwenda katika swala ya Ijumaa.