- Umuhimu wa utulivu na kuhudhurisha moyo ndani ya sala, na kuwa Shetani anajitahidi kutia tashiwishi na shaka ndani yake.
- Sunna ya kutaka ulinzi kutokana na shetani wakati wa wasi wasi wake ndani ya sala, pamoja na kutema kushoto mara tatu.
- Kumebainishwa waliyokuwa nayo Masahaba -Radhi za Allah ziwe juu yao- katika swala la kurudi kwao kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- katika yale yanayojitokeza kwao miongoni mwa changamoto ili azitatue.
- Maisha ya nyoyo za Masahaba, na kwamba hima yao kubwa ilikuwa ni Akhera.