- Ni wajibu kupandisha maji puani wakati wa udhu, nako ni: Kuingiza maji puani kwa njia ya pumzi, na pia ni wajibu kuyapenga, nako ni: Kuyatoa maji puani kwa njia ya pumzi.
- Inapendeza kupenga kwa witiri.
- Ni sheria kuosha mikono miwili baada ya kutoka usingizini mara tatu.