- Maana ya kushuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah, ni kumfanya Allah kuwa wa pekee kwa ibada, na kuacha kuabudu visivyokuwa Yeye.
- Maana ya kushuhudia kuwa Muhammad ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu; Ni kumuamini yeye na yale aliyokuja nayo na kumsadikisha, nakuwa yeye ni wa mwisho katika Wajumbe wa Mwenyezi Mungu kuja kwa wanadamu.
- Nikuwa kujadiliana na msomi mwenye hoja tata si sawa na kujadiliana na mjinga; Ndio maana alimtanabahisha Muadhi kwa kumwambia: "Hakika wewe unakwenda katika jamii ya watu wa kitabu".
- Kuna umuhimu wa muislamu kuwa na uelewa katika dini yake; ili asalimike na upotovu wa wenye kumtia utata, na hii inakuwa kwa kutafuta elimu.
- Ubatili wa dini ya Mayahudi na Wakristo baada ya kutumwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-, nakuwa wao si miongoni mwa watakao okoka siku ya Kiyama mpaka waingie katika dini Uislamu, na wamuamini Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-.