- Kumethibitishwa kuteremka kwa Issa amani iwe juu yake zama za mwisho, nakuwa tukio hilo ni katika alama za Kiyama.
- Sheria ya Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- haitofutwa na sheria yoyote.
- Kuteremka kwa baraka katika mali zama za mwisho, na watu kutoipenda.
- Habari njema ya kubakia kwa dini ya Uislamu kiasi ambacho Issa amani iwe juu yake atawahukumu watu zama za mwisho.