- Habari kuhusu kutokea ugeni wa Uislamu baada ya kuenea kwake na umaarufu wake.
- Hapa kuna alama miongoni mwa alama za utume, kiasi kwamba ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake yale yatakayotokea baada yake, na ikatokea kama alivyoeleza.
- Fadhila ya atakayehama nchi yake na familia yake; na kwamba atakuwa na Pepo.
- Wageni ni wale wanaotengemaa watu wanapoharibika, nao ni wale wanaorekebisha yale waliyoyaharibu watu.