- Tahadhari ya kujifananisha na makafiri na waovu.
- Himizo la kujifananisha na watu wema na kuiga kutoka kwao.
- Kujifananisha katika muonekano hutia mapenzi katika moyo.
- Mtu hupata kemeo la adhabu na madhambi kulingana na namna ya kujifananisha na aina yake.
- Katazo la kujifananisha na makafiri katika dini yao na katika desturi zao mahususi kwao, ama yasiyokuwa hayo kama kujifunza ufundi na mfano wake hayaingii katika katazo.