- Ubora wa Ally bin Abi Twalib – Mwenyezi Mungu amuwie radhi – na ushahidi wa Mtume – Mwenyezi Mungu amfikishie rehema na amani – juu yake, wa mapenzi ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake juu yake, na mapenzi yake kwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake.
- Maswahaba walikuwa na shauku ya kufanya kheri na kulikimbilia kwao hilo.
- Sheria ya adabu wakati wa vita na kuacha kutojali na kelele zenye kuudhi yasiyokuwa ya lazima.
- Miongoni mwa dalili za utume wake, rehema na amani ziwe juu yake, ni kutoa habari ya ushindi dhidi ya Mayahudi, na kumponya kwake macho Ally bin Abi Twalib mikononi mwake, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.
- Madhumuni makubwa ya Jihadi ni watu kuingia katika Uislamu.
- Nikuwa wito wa kuwaita watu katika Uislamu hutolewa taratibu taratibu, kwanza kafiri ataombwa kusilimu kwa kutamka Shahada mbili, kisha ataamrishwa kutekeleza faradhi za Uislamu baada ya hapo.
- Fadhila za kuwaita watu katika Uislamu na kheri zilizomo kwa mlinganiwaji na mlinganiaji, mlinganiwaji anaweza kuongoka, na mlinganiaji kwa hilo atalipwa malipo makubwa.