- Umuhimu wa kuamrisha mema na kukataza maovu katika kuzihifadhi jamii na kusalimika kwake.
- Miongoni mwa njia ya ufundishaji ni kupiga mifano, kwa ajili ya kusogeza uelewa wa akili kwa picha ya kitu chenye kueleweka.
- Kufanya uovu kwa wazi na kuto kukemea madhara yake yanarudi katika jamii nzima.
- Kuangamia kwa jamii kunaambatana na kuwaacha waovu wakiendelea kutapakaza maovu katika Ardhi.
- Kufanya mambo kimakosa na nia ikawa njema hili halitoshi kurekebisha matendo.
- Majukumu katika jamii ya kiislamu ni ya watu wote, hayaegemezwi kwa mtu maalum.
- Kuadhibiwa kwa watu wote kwa sababu ya madhambi ya wachache, ikiwa hayatokemewa.
- Waovu hudhihirisha maovu yao kwa sura ya kheri katika jamii kama walivyo wanafiki.