- Hadithi hii ni katika dalili za utume wake Rehema na amani ziwe juu yake, kiasi ambacho alieleza mambo yatakayotokea ndani ya Umma wake na yakatokea kama alivyoeleza.
- Inafaa kumueleza mtahiniwa yale yatakayomsibu katika mitihani; ili aitulize nafsi yake, mtihani ukimfika atakuwa na subira na atataraji malipo toka kwa Allah.
- Kushikamana na Qur'ani na Sunna ni sababu ya kutoka katika fitina na hitilafu.
- Himizo la kuwa wasikivu na watiifu kwa viongozi katika mema, na kutojitoa katika utiifu, hata kama zitatokea kwao dhulma.
- Kutumia hekima na kufuata mafundisho ya Mtume wakati wa fitina.
- Ni jukumu la kila mtu kutimiza haki ya msingi inayomlazimu hata kama itatokea kadhulumiwa.
- Hadithi inaashiria kanuni ya msingi ambayo ni: Mtu kuchagua moja kati ya shari mbili au madhara yenye nafuu.