- Uharamu wa kuwatuhumu watu kwa ukafiri au uovu, pasina sababu ya kisheria.
- Ulazima kupata uhakika katika utoaji wa hukumu kwa watu.
- Amesema bin Daqiq Al-Iddi: Na hii ni tahadhari kubwa kwa atakayemkufurisha yeyote katika waislamu haliyakuwa hayuko hivyo, na huku ni kujitia mtegoni kukubwa.
- Amesema bin Hajari Al-Asqalaani: Lakini haipelekei kutokuwa kwake muovu au kafiri kutokupata dhambi katika sura ya kauli yake: Wewe ni muovu, bali katika sura hii kuna mchanganuo: Ikiwa atakusudia kumnasihi au kumnasihi mtu mwingine kwa kubainisha hali yake hapa itafaa, na ikiwa atakusudia kumuaibisha na kumtangaza kwa hilo na kumuudhi haitafaa; kwa sababu ameamrishwa na sheria kumsitiri na kumueleimisha na kumpa mawaidha kwa njia nzuri, kwa namna yoyote itakayowezekana kwake kuitumia kwa upole basi haifai kwake kutumia ukali; kwa sababu inaweza kuwa sababu ya kumhadaa na kumfanya aendelee na hilo, kama ilivyo tabia ya baadhi ya watu pale upole usipotumika, na hasa hasa atapokuwa muamrishaji yuko chini ya muamriwa katika cheo.