Dhikiri bora ni: Laa ilaaha Illa llaah: Na dua bora ni: Al-hamdulillah
Imepokelewa Kutoka kwa Jabiri -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- akisema: "Dhikiri bora ni: Laa ilaaha Illa llaah: Na dua bora ni: Al-hamdulillah".
Ufafanuzi
Anatueleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa dhikiri bora ni: "Laa ilaaha illa llaah" Na maana yake, hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa dua bora ni "Al-hamdulillaah"; Nayo inamaanisha kukiri kuwa mneemeshaji ni Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka-, mwenye kustahiki sifa nzuri zilizokamilika.
Hadeeth benefits
Himizo la kukithirisha kumtaja Allah kwa neno la tauhidi (Laa ilaaha illa llaah), na kuomba kupitia himidi (Shukurani kwa Allah).
Share
Use the QR code to easily share the message of Islam with others