- Twahara zipo aina mbili: Twahara ya nje nayo ni udhu na kuoga, na twahara ya ndani inakuwa kwa kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kuwa na imani na matendo mazuri.
- umuhimu wa kuzihifadhi swala tano, kwakuwa swala tano ni mwangaza kwa mja hapa Duniani na siku ya Kiyama.
- Kutoa sadaka ni dalili ya imani ya kweli.
- Umuhimu wa kuifanyia kazi Qur'ani na kuisadikisha ili iwe ni hoja kwako au dhidi yako.
- Ikiwa nafsi hutoishughulisha na utiifu itakushughulisha na maasi.
- Kila mwanadamu lazima afanye matendo, hivyo ima aikomboe nafsi yake kwa kutii, au aiangamize kwa kufanya maasi.
- Na subira inahitaji uvumilivu na kutarajia thawabu, na ndani yake kuna uzito.