- Kumtegemea Mwenyezi Mungu Mtukufu, nakuwa hakuna awezaye kuleta kheri isipokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna awezaye kuzia shari isipokuwa Mwenyezi Mungu.
- Katazo la kuamini mikosi ya ndege, nayo ni kila kitu kinachoaminika kuwa ni mkosi, na kufanya kazi isifanyike.
- Matumaini si katika mikosi iliyokatazwa, bali ni katika kumdhania kheri Mwenyezi Mungu Mtukufu.
- Kila kitu kinachotokea ni kwa mipango na makadirio ya Mwenyezi Mungu Mtukufu peke yake, yeye pekee asiye na mshirika wake.