- Malipo huwa kwa mujibu wa matendo, kwa kuangalia wingi wake na namna yalivyofanywa.
- Himizo juu ya kuisoma Qur'ani kwa namna nzuri na kuihifadhi na kuizingatia pamoja na kuifanyia kazi.
- Pepo ina vituo na daraja nyingi, watu wa Qur'ani hupata daraja la juu kabisa.