- Ni lazima kushikamana na dini, na kwenda mbio katika matendo mema kabla ya vikwazo kuzuia hilo.
- Hii ni ishara ya mfuatano wa majaribu yenye kupoteza katika zama za mwisho, na kwamba wakati wowote fitina moja inapotoweka, fitina ingine linafuata.
- Ikiwa dini ya mtu ni dhaifu na akaiacha kwa kubadilishana na mambo ya kidunia, kama vile pesa au vitu vingine, hii ni sababu ya kupotoka kwake, kuacha dini, na kuingia kwake kwenye vishawishi na fitina.
- Kuna ushahidi katika Hadithi kwamba matendo mema ni njia ya kuokoka na fitina.
- Kuna aina mbili za fitina: Fitina ya shubuha (Mambo yenye utata), na tiba yake ni elimu, na fitina ya matamanio, na tiba yake ni imani na subira.
- Hadithi inaashiria kuwa mwenye matendo kidogo, fitina kwake ni nyepesi zaidi, na mwenye matendo mengi anatakiwa asihadaike na alichonacho, bali aongeze zaidi.