- Miongoni mwa huruma ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake waumini ni kuwafutia madhambi yao katika dunia yao kupitia matatizo ya dunia na maafa yake.
- Balaa pekee linafuta madhambi ila kwa sharti la imani, hivyo akisubiri mja na akawa hakulalamika basi analipwa.
- Himizo la subira katika mambo yote, katika yale ayapendayo na anayoyachukia, awe na subira mpaka atekeleze aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu, na awe na subira mpaka akae mbali na yale aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu, akitaraji malipo ya Mwenyezi Mungu na kuogopa adhabu yake.
- Kauli yake: “Kwa muumini mwanaume na mwanamke,” kuongeza neno “muumini wa kike” ndani yake ni ushahidi wa kutiliwa mkazo zaidi kwa wanawake. Vinginevyo, lau angesema: "Kwa muumini wa kiume," mwanamke angejumuishwa ndani yake; Kwa sababu hii si mahsusi kwa wanaume, basi ikiwa dhiki itampata mwanamke, naye anaahidiwa malipo kama hayo kwa kufutiwa madhambi na makosa.
- Hili ni miongoni mwa mambo yanayomtia faraja mtu kwa yale anayokumbana nayo katika maumivu kila mara yanayosababishwa na mabalaa.