- Wepesi na urahisi wa sheria ya Uislamu, na kuwa kwake ya kati na kati, kati ya uzembe na mkazo.
- Mja analazimika kufanya matendo kwa kadiri ya uwezo wake, pasina kupuuza au kutia mkazo.
- Ni lazima mja achague nyakati za kuwa na uchangamfu katika ibada, na nyakati hizi tatu ndizo nyakati bora ambazo mwili unakuwa na uchangamfu katika ibada.
- Amesema bin Hajar Al-Asqalani: Ni kana kwamba rehema na amani ziwe juu yake amemuelekeza msafiri mahali pa kupelekwa, na nyakati hizi tatu ndizo nyakati bora kwa msafiri, hivyo akamzindua nyakati za uchangamfu wake; Kwa sababu ikiwa msafiri atasafiri mchana na usiku mzima, atakuwa hana uwezo na akakatikiwa, na ikiwa atajitahidi kutembea katika nyakati hizi za uchangamfu basi ataweza kudumu bila tabu.
- Amesema bin Hajar: Hadithi hii inaashiria kuchukua ruhusa ya kisharia, kwa sababu kufanya ulazima mahali pa ruhusa ni ukiukaji, sawa na mtu anayeacha tayammam wakati hana uwezo wa kutumia maji na kuyatumia kwake kukapelekea kuleta madhara.
- Amesema bin Munir: Hadithi hii ni miongoni mwa alama za unabii, kwa hakika tuliona na watu waliotangulia pia waliona kuwa kila mwenye kupita kiasi katika dini huishia njiani, na makusudio yake si kuzuia kutaka ukamilifu katika ibada, kwani ni katika mambo ya kusifiwa, bali ni kuzuia uzembe unaopelekea katika uvivu, au kupita mipaka katika jambo la sunna kunakopelekea kuacha kilicho bora, au kuitoa faradhi nje ya wakati wake, kama vile mtu aliyekesha usiku kucha kisha akalala na akapitwa na Swala ya Alfajiri kwa jamaa, au mpaka jua likachomoza na muda wa kuswali ukatoka.