- Umuhimu wa kuihifadhi swala ya jamaa msikitini, na kuzipa kipaumbele swala na kutozipuuza.
- Uzuri wa uwasilishaji wake Mtume rehema na amani ziwe juu yake wa mada na kuwatia kwake hamu Maswahaba zake, kwani alianza kuwatajia ujira mkubwa kwa njia ya kuuliza swali, na hii ni njia mojawapo ya ufundishaji.
- Faida ya kuwasilisha suala kwa maswali na majibu: Ili mazungumzo yakite ndani ya nafsi kwa sababu ya utata wake kisha kuyatolea ufafanuzi.
- Amesema An-Nawawi, Mwenyezi Mungu amrehemu: Hiyo ndio Jihadi: Maana yake ni Jihadi iliyohimizwa, na asili ya neno (Ribat) ni kufunga kitu, kana kwamba mtu amejifunga kwa ajili ya ibada hizi, na imesemwa kuwa: Ni Jihadi bora, kama ilivyosemwa: Jihadi ni jihadi ya nafsi, na inawezekana kuwa ni Jihadi nyepesi inayowezekana, yaani: ni aina mojawapo ya Jihadi.
- Neno “Ribat” lilirudiwa na kufafanuliwa kwa ufafanuzi (Alif na Lam); Hii ni kwa ajili ya utukufu wa matendo haya.