- Kuingia peponi hakui ila kwa imani.
- Katika ukamilifu wa imani ni muislamu kumpendelea muislamu mwenzake yale anayoyapenda yeye.
- Ni sunna kutoa salam na kuisambaza kwa waislamu; kwa sababu kuisambaza ni kusambaza mapenzi na amani baina ya watu.
- Salam haitolewi ila kwa muislamu; kwa kauli yake Rehema na amani ziwe juu yake: "Baina yenu".
- Kutoa salam kunaondoa chuki na kuhamana na vifundo.
- Umuhimu wa mapenzi kati ya waislamu nakuwa hilo ni katika ukamilifu wa imani.
- Imekuja katika hadithi nyingine kuwa namna ya salam kamili ni: "As-salaam alaikum warahmatullahi wabarakaatuh", na inatosha: "Assalaam alaikum".