- Ubora wa Abubakari -Radhi za Allah ziwe juu yake-, nakuwa yeye ndiye Swahaba bora na mtu bora kwa kuushika ukhalifa wa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- baada ya kifo chake.
- Kujenga misikiti juu ya makaburi ni katika maovu ya umma zilizopita.
- Katazo la kuyafanya makaburi kuwa sehemu za ibada kwa ajili ya kuswalia hapo au kuyaelekea na kujengwa juu yake misikiti au makuba, kwa tahadhari ya kutoangukia katika ushirikina kwa sababu ya hilo.
- Tahadhari ya kuchupa mipaka kwa watu wema, kwani hupelekea kwenye ushirikina.
- Uhatari wa yale aliyoyatahadharisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kiasi kwamba aliyatilia mkazo kabla ya kifo chake kwa siku tano.