- Uharamu wa kujenga Misikiti juu ya makaburi, au kuswali hapo, au kuzika maiti ndani ya msikiti; hii ikiwa ni kuziba njia za kuelekea katika ushirikina.
- Kujenga Misikiti juu ya makaburi, na kutundika picha, hiki ni kitendo cha Mayahudi, nakuwa mwenye kufanya hivi atakuwa kafanana nao.
- Uharamu wa kutengeneza picha za viumbe hai (wenye roho).
- Atakayejenga msikiti juu ya kaburi na akachoro ndani yake picha, huyu ni katika viumbe waovu zaidi kuliko wote mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.
- Sheria imeuhami sana upande wa tauhidi kwa himaya iliyokamilika, kwa kuziba njia zote ambazo zinaweza kusababisha kufika katika ushirikina.
- Katazo la kuchupa mipaka kwa watu wema; kwani ni sababu ya kuingia katika shirki.