- Huruma ya Mwenyezi Mungu na upole wake kwa viumbe.
- Wema wa kuuwa na kuchinja uwe kwa namna ya kisheria.
- Ukamilifu wa sheria na kushughulikia kwake kila kheri, na miongoni mwake ni kuwahurumia wanyama na upole juu yao.
- Katazo la kusulubu (kumtesa) mwanadamu baada ya kumuua.
- Uharamu wa kila chenye kumtesa mnyama.