- Sheria ya kuchinja siku ya Idi kubwa (Adh-ha), na waislamu wote wamekubaliana hilo.
- Kilichobora zaidi ni kuwa kichinjwa kiwe cha aina hii aliyochinja Mtume rehema na amani ziwe juu yake; kwa muonekano wake mzuri lakini pia mafuta yake na nyama yake nzuri.
- Amesema Imam Nawawi: Hapa kuna sunna ya mtu asimamie mwenyewe kuchinja kichinjwa chake cha udhuhia, na wala asimuwakilishe yeyote ila kwa udhuru, na hapo pia ni sunna ashuhudie kichinjwa chake, na ikiwa atamuweka muislamu kwa niaba yake itafaa kwa itifaki ya wanachuoni.
- Amesema bin Hajari: Na hapa kuna sunna ya kutoa takbira (Allaahu Akbaru) pamoja na kumtaja Mwenyezi Mungu (Bismillaah) wakati wa kuchinja, na kuweka mguu katika weupe wa shingo wa kulia wa mnyama, na wamekubaliana wanachuoni kuwa ubavu wake unakuwa upande wa kushoto ataweka mguu wake wa kulia ili iwe rahisi kumchinja wakati wa kuchukua kisu kwa mkono wa kulia na kukamata kichwa chake kwa mkono wake wa kulia
- Ni sunna kichinjwa cha udh-hiya kiwe na pembe na inafaa pia kwa kinginecho.