- Uwajibu wa kutekeleza sharti ambazo amezitilia umuhimu mmoja kati ya wanandoa wawili kwa mwenzie, isipokuwa sharti itakayoharamisha halali au kuhalalisha haramu.
- Kutekeleza sharti za ndoa kumetiliwa mkazo kuliko sharti zote; kwa sababu huambatana na kuhalalisha tupu.
- Ukubwa wa nafasi ya ndoa katika Uislamu, kiasi ambacho umetilia mkazo juu ya kutimiza sharti zake.