- Kuunga udugu kunakozingatiwa kisheria ni kumuunga aliyekukata miongoni mwao, na kumsamehe aliyekudhulumu, na kumpa aliyekunyima, na si kuunga udugu kwa kubadilishana (wakiniunga nitawaunga wakikata nawakata) au kulipa wema uliotendewa.
- Kuunga udugu kunakuwa kwa kufikisha kheri kwa kadiri ya uwezo, kwa kutumia mali na dua na kuamrishana mema na kukatazana maovu na mfano wake, na kuzuia yawezekanayo katika shari juu yao.