Hakika Mwenyezi Mungu hupata wivu, na hakika muumini hupata wivu, na wivu wa Mwenyezi Mungu ni pale muumini anapoyafanya yale aliyomharamishia juu yake
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -sala na amani ziwe juu yake-: "Hakika Mwenyezi Mungu hupata wivu, na hakika muumini hupata wivu, na wivu wa Mwenyezi Mungu ni pale muumini anapoyafanya yale aliyomharamishia juu yake".
Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Ufafanuzi
Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa Mwenyezi Mungu hupata wivu na huchukia na hukarahika, kama ambavyo muumini hupata wivu na huchukia na kukarahika, nakuwa sababu ya wivu wa Mwenyezi Mungu ni pale muumini anapoyafanya yale aliyomharamishia Mwenyezi Mungu juu yake miongoni mwa machafu kama zinaa liwati (Ushoga na ubasha) wizi na kunywa pombe na mengineyo katika machafu.
Hadeeth benefits
Kutahadhari na hasira na ghadhabu za Mwenyezi Mungu na adhabu yake pale yanapofanywa maharamisho yake.
Share
Use the QR code to easily share the message of Islam with others