- Himizo na kufaidika na nyakati bora kwa matendo mema.
- Amesema Nawawi: Na katika hadithi hii: Nikuwa inapendeza kuzidisha katika ibada mbali mbali katika siku kumi za mwisho wa Ramadhani, na kupendeza kuhuisha siku zake kwa ibada mbali mbali.
- Yampasa kila mja awe na pupa kwa familia yake ya kuwaamrisha kufanya ibada, na awe mvumilivu juu yao.
- Kufanya mambo ya heri kunahitaji uthubutu na subira na kuvumilia.
- Amesema Nawawi: Wametofautiana wanachuoni katika maana ya (Kukaza kikoi) wakasema: Ni kuongeza juhudi katika ibada zaidi ya kawaida yake Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika nyakati zingine, na maana yake: Ni kujipinda katika ibada, husemwa: Jambo hili nimelifungia kikoi, yaani: Nimelidhamiria na nimetenga muda wangu kwa ajili yake, na wamesema wengine: Ni fumbo la kujitenga na wanawake kwa ajili ya kushughulika na ibada.