Allah amhurumie mtu ambaye ni mpole anapouza, na anaponunua, na anapo dai deni
Imepokelewa Kutoka kwa Jabiri -Radhi za Allah ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema: "Allah amhurumie mtu ambaye ni mpole anapouza, na anaponunua, na anapo dai deni".
Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Ufafanuzi
Alimuombea rehema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kila mwenye kuwa mwepesi mkarimu mpole katika biashara yake; Hamkadamizi mnunuzi katika bei yake, na anaamiliana naye kwa tabia njema, Mwepesi mkarimu mpole anaponunua; Hapunji na kupunguza thamani ya bidhaa, Mwepesi mkarimu mpole anapodai kulipwa madeni yake; hamtilii mkazo fukara na muhitaji, bali anamdai kwa upole na huruma, na anampa muda mwenye hali ngumu.
Hadeeth benefits
Miongoni mwa malengo ya sheria ni kuhifadhi yenye kutengeneza mahusiano baina ya watu.
Himizo la kutumia tabia za hali ya juu katika miamala baina ya watu kuanzia kuuza na kununuwa na mfano wake.
Share
Use the QR code to easily share the message of Islam with others